16
1 #
Mt 10:19; Mit 19:21 Mipango ya moyoni ni ya mwanadamu,
bali jibu la ulimi hutoka kwa Bwana.
2 #
1Sam 16:7; 2Nya 6:30; Lk 16:15; Dan 5:27 Njia zote za mtu huonekana safi machoni pake mwenyewe,
bali makusudi hupimwa na Bwana.
3 #
2Nya 20:20; Za 20:4 Mkabidhi Bwana lolote ufanyalo,
nayo mipango yako itafanikiwa.
4 #
Isa 43:7; Kut 9:16; 2Nya 34:24; Rum 9:22 Bwana hufanya kila kitu kwa kusudi lake mwenyewe;
hata waovu kwa siku ya maangamizi.
5 #
Za 40:4; Mit 6:16; 11:20-21 Bwana huwachukia sana wote wenye kiburi cha moyo.
Uwe na hakika kwa hili: Hawataepuka kuadhibiwa.
6 #
Kut 20:20; Mit 14:16; Dan 4:26 Kwa upendo na uaminifu uovu huondolewa;
kwa kumcha Bwana mtu hujiepusha na ubaya.
7 #
Kol 1:10; Mwa 39:21; Za 105:15; Yer 39:12; 40:1; 42:12; Dan 1:9 Njia za mtu zinapompendeza Bwana,
huwafanya hata adui zake waishi naye kwa amani.
8 #
Za 37:16; Mit 15:16; 17:1; Mhu 4:6 Afadhali kitu kidogo pamoja na haki
kuliko mapato mengi pamoja na udhalimu.
9 #
Yer 10:23
Moyo wa mtu huifikiri njia yake,
bali Bwana huelekeza hatua zake.
10 #
Mit 17:7
Midomo ya mfalme huzungumza kwa hekima ya kiungu,
wala kinywa chake hakipotoshi haki.
11 #
Law 19:36; Mit 11:1; Eze 45:10 Vipimo na mizani za halali hutoka kwa Bwana;
mawe yote ya kupimia yaliyo katika mfuko ameyafanya yeye.
12 #
Mit 26:28; 25:5; 29:14; 31:5 Wafalme huchukia sana kutenda maovu,
kwa maana kiti cha ufalme hufanywa imara kwa njia ya haki.
13 #
Mit 22:11
Wafalme hufurahia midomo ya uaminifu;
humthamini mtu asemaye kweli.
14 #
Mwa 40:2; Ay 29:24 Ghadhabu ya mfalme ni mjumbe wa mauti,
bali mtu mwenye hekima ataituliza.
15 #
2Nya 36:16; Mit 29:1; Yer 19:11 #
Mwa 40:2; Ay 29:24; Mit 19:12; 25:2-7 Uso wa mfalme ungʼaapo, inamaanisha uhai;
upendeleo wake ni kama wingu la mvua wakati wa vuli.
16 #
Za 49:20; Ay 28:15; Mit 3:13-14 Ni bora kiasi gani kupata hekima kuliko dhahabu,
kuchagua ufahamu kuliko fedha!
17 #
Mit 4:24-27; Isa 35:8; Mdo 24:16 Njia kuu ya wanyofu huepuka ubaya;
yeye aichungaye njia yake, huchunga maisha yake.
18 #
Es 5:12; Mit 29:23 Kiburi hutangulia maangamizi,
roho ya majivuno hutangulia maanguko.
19Ni afadhali kuwa mnyenyekevu katika roho
miongoni mwa walioonewa
kuliko kugawana nyara pamoja na wenye kiburi.
20 #
Isa 30:18; Za 32:10; Yer 17:7 Yeyote anayekubali mafundisho hustawi,
tena amebarikiwa yeye anayemtumaini Bwana.
21 #
Mit 16:23
Wenye hekima moyoni huitwa wenye ufahamu,
na maneno ya kupendeza huchochea mafundisho.
22 #
Mit 10:11
Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwa wale walio nao,
bali upumbavu huleta adhabu kwa wapumbavu.
23 #
Ay 15:5; Mit 16:21 Moyo wa mtu mwenye hekima huongoza kinywa chake,
na midomo yake huchochea mafundisho.
24 #
Mit 24:13-14
Maneno ya kupendeza ni kama sega la asali,
ni matamu kwa nafsi na uponyaji kwenye mifupa.
25 #
Mit 12:15; 14:12; Es 3:6 Iko njia ionekanayo kuwa sawa kwa mtu,
bali mwisho wake huelekeza mautini.
26 #
Mit 9:12; Mhu 6:7 Shauku ya mfanyakazi humhimiza kufanya kazi;
njaa yake humsukuma aendelee.
27 #
Yak 3:6
Mtu mbaya kabisa hupanga mabaya,
maneno yake ni kama moto uunguzao.
28 #
Mit 14:17; 17:9 Mtu mpotovu huchochea ugomvi,
nayo maongezi ya upuzi hutenganisha marafiki wa karibu.
29Mtu mkali humvuta jirani yake
na kumwongoza katika mapito yale mabaya.
30 #
Mit 6:13
Yeye akonyezaye kwa jicho lake anapanga upotovu;
naye akazaye midomo yake amenuia mabaya.
31 #
Mit 20:29
Mvi ni taji ya utukufu;
hupatikana kwa maisha ya uadilifu.
32 #
Mit 19:11
Ni afadhali mtu mstahimilivu kuliko shujaa,
mtu anayeitawala hasira yake kuliko yule autekaye mji.
33 #
Yos 7:14; Yn 1:7 Kura hupigwa kwa siri,
lakini kila uamuzi wake hutoka kwa Bwana.