Mithali 2
NEN

Mithali 2

2
Faida Za Hekima
1 # Mit 1:8 Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu
na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,
2 # Mit 22:17 kutega sikio lako kwenye hekima
na kuweka moyo wako katika ufahamu,
3 # Yak 1:5 na kama ukiita busara
na kuita kwa sauti ufahamu,
4 # Ay 3:21; Mt 13:44; 6:19-21 na kama utaitafuta kama fedha
na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,
5 # Kum 4:6 ndipo utakapoelewa kumcha Bwana
na kupata maarifa ya Mungu.
6 # Ay 12:13; Lk 21:15; Yak 1:5 Kwa maana Bwana hutoa hekima,
na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.
7 # Mwa 6:9; 15:1; Mit 30:5-6; Za 84:11 Anahifadhi ushindi kwa ajili ya mwadilifu,
yeye ni ngao kwa wale wasio na lawama,
8 # 1Sam 2:9; Za 18:25 kwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki
na kuhifadhi njia ya waaminifu wake.
9 # Kum 1:16 Ndipo utafahamu lipi lililo kweli na haki
na sawa: yaani kila njia nzuri.
10 # Mit 14:33 Kwa maana hekima itaingia moyoni mwako,
nayo maarifa yataifurahisha nafsi yako.
11 # Mit 4:6 Busara itakuhifadhi
na ufahamu utakulinda.
12 # Mit 2:16; 3:13-18; 4:5 Hekima itakuokoa kutoka njia za waovu,
kutoka kwa watu ambao maneno yao yamepotoka,
13 # Mit 4:19; Yn 3:19; Efe 4:18 wale waachao mapito yaliyonyooka
wakatembea katika njia za giza,
14 # Mit 15:21; Yer 11:15 wale wapendao kutenda mabaya
na kufurahia upotovu wa ubaya,
15 # Za 125:5; Mit 21:8 ambao mapito yao yamepotoka
na ambao ni wapotovu katika njia zao.
16 # Mit 6:20-29; 7:5-27 Itakuokoa pia kutokana na mwanamke kahaba,
kutokana na mke aliyepotoka mwenye maneno
ya kushawishi kutenda ubaya,
17 # Mal 2:14; Mwa 2:24 aliyemwacha mwenzi wa ujana wake
na kupuuza agano alilofanya mbele ya Mungu.
18 # Mit 5:5; 7:27; 9:18 Kwa maana nyumba yake huelekea kwenye kifo
na mapito yake kwenye roho za waliokufa.
19 # Mit 5:8; Mhu 7:26; Ebr 13:4 Hakuna yeyote aendaye kwake akarudi,
au kufikia mapito ya uzima.
20 # Ebr 6:12 Hivyo utatembea katika njia za watu wema
na kushikamana na mapito ya wenye haki.
21 # Za 37:29 Kwa maana wanyofu wataishi katika nchi,
nao wasio na lawama watabakia ndani yake.
22 # Ay 18:17; Za 37:38; Kum 29:28 Bali waovu watakatiliwa mbali kutoka nchi,
nao wasio waaminifu watangʼolewa kutoka humo.

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Biblia Takatifu)

Copyright ©1984, 1989, 2009, 2015 by Biblica, Inc.® Used by permission.

All Rights Reserved Worldwide Printed.

Learn More About Neno: Bibilia Takatifu 2014