7
Onyo Dhidi Ya Mwanamke Mzinzi
1 #
Mt 1:8
Mwanangu, shika maneno yangu
na kuzihifadhi amri zangu ndani yako.
2 #
Mit 4:4; Law 18:5; Kum 32:10 Shika amri zangu nawe utaishi;
linda mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.
3 #
Kum 6:8; Mit 3:3; Isa 30:8; 2Kor 3:3 Yafunge katika vidole vyako;
yaandike katika kibao cha moyo wako.
4Mwambie hekima, “Wewe ni dada yangu,”
uite ufahamu jamaa yako;
5 #
Ay 31:9; Mit 2:16 watakuepusha na mwanamke mzinzi,
kutokana na mwanamke mpotovu
na maneno yake ya kubembeleza.
6Kwenye dirisha la nyumba yangu
nilitazama nje kupitia upenyo
kwenye mwimo wa dirisha.
7 #
Mit 6:32
Niliona miongoni mwa wajinga,
nikagundua miongoni mwa wanaume vijana,
kijana asiye na akili.
8Alikuwa akishuka njiani karibu na pembe ya kwake,
akielekea kwenye nyumba ya huyo mwanamke
9 #
Ay 24:15
wakati wa machweo, jua likipungua nuru yake,
giza la usiku lilipokuwa likiingia.
10 #
1Tim 2:9
Ndipo huyo mwanamke akatoka kumlaki,
hali amevaa kama kahaba akiwa na nia ya udanganyifu.
11 #
Mit 9:13; 1Tim 5:13 (Ni mwanamke mwenye makelele na mkaidi,
miguu yake haitulii nyumbani;
12 #
Mit 8:1-36; 23:26-28 mara kwenye barabara za mji,
mara kwenye viwanja vikubwa,
kwenye kila pembe huvizia.)
13 #
Mwa 39:12; Mit 1:20 Huyo mwanamke alimkumbatia kijana na kumbusu,
na kwa uso usio na haya akamwambia:
14 #
Law 7:11-18
“Nina sadaka za amani nyumbani;
leo nimetimiza nadhiri zangu.
15Kwa hiyo nimetoka nje kukulaki;
nimekutafuta na nimekupata!
16 #
Isa 19:9
Nimetandika kitanda changu
kwa kitani za rangi kutoka Misri.
17 #
Amo 6:4; Mwa 37:25 Nimetia manukato kitanda changu
kwa manemane, udi na mdalasini.
18 #
Mwa 39:7
Njoo, tuzame katika mapenzi mpaka asubuhi;
tujifurahishe wenyewe kwa mapenzi!
19Mume wangu hayupo nyumbani;
amekwenda safari ya mbali.
20Amechukua mkoba uliojazwa fedha
na hatakuwepo nyumbani karibuni.”
21 #
Mit 1:8-9; 8:32 Kwa maneno laini yule mwanamke akampotosha;
alimshawishi kwa maneno yake laini.
22 #
Ay 18:10
Mara huyo kijana alimfuata yule mwanamke
kama fahali aendaye machinjoni,
kama kulungu aingiaye kwenye kitanzi,
23 #
Ay 15:22; 16:13; Mit 6:26; Mhu 9:12 mpaka mshale umchome ini lake,
kama ndege anayenaswa kwenye mtego,
bila kujua itamgharimu maisha yake.
24 #
Mit 1:8-9; 8:32 Sasa basi wanangu, nisikilizeni;
sikilizeni kwa makini nisemalo.
25 #
Mit 5:7-8
Usiruhusu moyo wako ugeukie njia za huyo mwanamke,
wala usitangetange katika mapito yake.
26 #
Neh 13:26
Aliowaangusha ni wengi;
aliowachinja ni kundi kubwa.
27 #
Amu 16:19; Ufu 22:15 Nyumba yake ni njia kuu iendayo kaburini,#7:27 Kaburini hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol.
ielekeayo chini kwenye vyumba vya mauti.