Zaburi 114
NEN

Zaburi 114

114
Zaburi 114
Maajabu Ya Mungu Wakati Israeli Walipotoka Misri
1 # Kut 13:3; 29:46 Wakati Israeli walipotoka Misri,
nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
2 # Kut 15:17; Za 76:1; 78:68, 69 Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu,
Israeli akawa milki yake.
3 # Kut 14:21; Za 77:16; Kut 15:8; Yos 3; 16 Bahari ilitazama ikakimbia,
Yordani ulirudi nyuma,
4 # Amu 5:5 milima ilirukaruka kama kondoo dume,
vilima kama wana-kondoo.
5 # Kut 14:21 Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia,
nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
6enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume,
enyi vilima, kama wana-kondoo?
7 # Kut 15:14; 1Nya 16:30 Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana,
mbele za Mungu wa Yakobo,
8 # Kut 17:6; Hes 20:11 aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji,
mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Biblia Takatifu)

Copyright ©1984, 1989, 2009, 2015 by Biblica, Inc.® Used by permission.

All Rights Reserved Worldwide Printed.

Learn More About Neno: Bibilia Takatifu 2014