Zaburi 121
NEN

Zaburi 121

121
Zaburi 121
Bwana Mlinzi Wetu
Wimbo wa kwenda juu.
1Nayainua macho yangu nitazame vilima,
msaada wangu utatoka wapi?
2 # Mwa 1:1; Za 104:5 Msaada wangu hutoka kwa Bwana,
Muumba wa mbingu na dunia.
3 # 1Sam 2:9; Isa 27:3 Hatauacha mguu wako uteleze,
yeye akulindaye hatasinzia,
4 # Za 127:1 hakika, yeye alindaye Israeli
hatasinzia wala hatalala usingizi.
5 # Za 1:6 Bwana anakulinda,
Bwana ni uvuli wako mkono wako wa kuume,
6 # Isa 49:10 jua halitakudhuru mchana,
wala mwezi wakati wa usiku.
7 # Za 9:9, 10; 91:9, 10; Ay 5:19; Mit 12:21 Bwana atakukinga na madhara yote,
atayalinda maisha yako,
8 # Kum 28:6; Mit 2:8 Bwana atakulinda unapoingia na unapotoka,
tangu sasa na hata milele.

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Biblia Takatifu)

Copyright ©1984, 1989, 2009, 2015 by Biblica, Inc.® Used by permission.

All Rights Reserved Worldwide Printed.

Learn More About Neno: Bibilia Takatifu 2014