Zaburi 129
NEN

Zaburi 129

129
Zaburi 129
Maombi Dhidi Ya Adui Za Israeli
Wimbo wa kwenda juu.
1 # Kut 1:13; Eze 23:3; Za 88:15; 124:1; Hos 2:15 Wamenionea mno tangu ujana wangu;
Israeli na aseme sasa:
2 # Yer 1:19; 15:20; 20:11 wamenionea mno tangu ujana wangu,
lakini bado hawajanishinda.
3 # Ebr 11:26 Wakulima wamelima mgongo wangu,
na kufanya mifereji yao mirefu.
4 # Kut 9:27; 2The 1:6; Za 37:9; 140:5 Lakini Bwana ni mwenye haki;
amenifungua toka kamba za waovu.
5 # Mik 4:11; Za 70:2 Wale wote waichukiao Sayuni
na warudishwe nyuma kwa aibu.
6 # Isa 37:27; 2Fal 19:26; Za 102:11; 37:2; Yer 17:5-6 Wawe kama majani juu ya paa,
ambayo hunyauka kabla hayajakua;
7 # Kum 28:38; Za 79:12 kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake,
wala akusanyaye kujaza mikono yake.
8 # Za 118:26; Rut 2:4 Wale wapitao karibu na wasiseme,
“Baraka ya Bwana iwe juu yako;
tunakubariki katika jina la Bwana.”

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Biblia Takatifu)

Copyright ©1984, 1989, 2009, 2015 by Biblica, Inc.® Used by permission.

All Rights Reserved Worldwide Printed.

Learn More About Neno: Bibilia Takatifu 2014