Zaburi 150
NEN

Zaburi 150

150
Zaburi 150
Msifuni Bwana Kwa Ukuu Wake
1 # Za 112:1; 73:17; 68:24-26; 102:19; 148:1 Msifuni Bwana.
Msifuni Mungu katika patakatifu pake,
msifuni katika mbingu zake kuu.
2 # Kum 3:24; Kut 15:7 Msifuni kwa matendo yake makuu,
msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.
3 # Hes 10:2; Za 57:8 Msifuni kwa mvumo wa tarumbeta,
msifuni kwa kinubi na zeze,
4 # Kut 15:20; Za 45:8; Isa 38:20; Mwa 4:21 msifuni kwa matari na kucheza,
msifuni kwa kinanda cha nyuzi na filimbi,
5 # 2Sam 6:5 msifuni kwa matoazi yaliayo,
msifuni kwa matoazi yavumayo sana.
6 # Za 103:22; Ufu 5:13 Kila chenye pumzi na kimsifu Bwana.
Msifuni Bwana!

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Biblia Takatifu)

Copyright ©1984, 1989, 2009, 2015 by Biblica, Inc.® Used by permission.

All Rights Reserved Worldwide Printed.

Learn More About Neno: Bibilia Takatifu 2014