55
Zaburi 55
Maombi Ya Mtu Aliyesalitiwa Na Rafiki
Kwa mwimbishaji. Na ala za uimbaji. Utenzi wa Daudi.
1 #
Za 27:9; Mao 3:56 Ee Mungu, sikiliza maombi yangu,
wala usidharau hoja yangu.
2 #
1Sam 1:15-16; Za 4:1; 77:3; 86:6-7; 142:2 Nisikie na unijibu.
Mawazo yangu yananisumbua na nimehangaishwa
3 #
2Sam 16:6-8; 17:9; Za 143:3; 44:16; 71:11 kwa sauti ya adui,
kwa kukaziwa macho na waovu,
kwa sababu wananiletea mateso juu yangu
na kunitukana kwa hasira zao.
4 #
Ay 18:11; Za 6:3; 102:3-5; Yn 12:27; Mt 26:37, 38; 2Kor 1:8-10 Moyo wangu umejaa uchungu,
hofu ya kifo imenishambulia.
5 #
Ay 4:14; Eze 7:18; 2Kor 7:15; Isa 21:4; Kum 28:67; Yer 46:5; 49:5 Woga na kutetemeka vimenizunguka,
hofu kuu imenigharikisha.
6Nilisema, “Laiti ningekuwa na mbawa za njiwa!
Ningeruka niende mbali kupumzika.
7 #
1Sam 23:14
Ningalitorokea mbali sana
na kukaa jangwani,
8 #
Za 31:20; 77:18; Isa 4:6; 25:4; 28:2; 29:6; 32:2 ningaliharakisha kwenda mahali pa salama,
mbali na tufani kali na dhoruba.”
9 #
Mwa 4:17; 11:9; Mdo 2:4; Za 11:5; Isa 59:6; Yer 6:7; Eze 7:11; Hab 1:3 Ee Bwana, uwatahayarishe waovu
na uwachanganyishie semi zao,
maana nimeona jeuri na ugomvi mjini.
10 #
1Pet 5:8
Usiku na mchana wanazunguka juu ya kuta zake,
uovu na dhuluma vimo ndani yake.
11 #
Za 5:9; 10:7 Nguvu za uharibifu zinatenda kazi mjini,
vitisho na uongo haviondoki mitaani mwake.
12Kama aliyenitukana ni adui yangu, ningevumilia,
kama mtu mwovu angejiinua dhidi yangu,
ningejificha asinione.
13 #
2Sam 15:12
Kumbe ni wewe, mwenzangu,
mshiriki na rafiki yangu wa karibu,
14 #
Mdo 1:16-17; Za 42:4 ambaye awali tulifurahia ushirika mzuri,
tulipokuwa tukienda na umati hekaluni mwa Mungu.
15 #
Za 64:7; 49:14; Mit 6:5; Isa 29:5; 47:9, 11; 1The 5:3; Hes 16:30 Kifo na kiwajie adui zangu ghafula,
na washuke kuzimu wangali hai,
kwa maana uovu upo ndani yao.
16Lakini ninamwita Mungu,
naye Bwana huniokoa.
17 #
Za 141:2; 88:13; 92:2; 5:3; Mdo 3:1; 10:9; 10:3, 30; Lk 18:1; Dan 6:10 Jioni, asubuhi na adhuhuri
ninalia kwa huzuni,
naye husikia sauti yangu.
18 #
2Nya 32:7
Huniokoa nikawa salama katika vita
vilivyopangwa dhidi yangu,
ingawa watu wengi hunipinga.
19 #
Kum 33:27; Za 29:10; 78:59; 36:1; 64:4; Kut 15:18 Mungu anayemiliki milele,
atawasikia na kuwaadhibu,
watu ambao hawabadilishi njia zao,
wala hawana hofu ya Mungu.
20 #
Za 7:4; 41:9 Mwenzangu hushambulia rafiki zake,
naye huvunja agano lake.
21 #
Za 59:7; 57:4; 12:2; 64:3; Ufu 1:16; Mit 5:3; 6:24; 12:18 Mazungumzo yake ni laini kama siagi,
hata hivyo vita vimo moyoni mwake.
Maneno yake ni mororo kuliko mafuta,
hata hivyo ni upanga mkali uliofutwa.
22 #
1Pet 5:7; Za 15:5; 18:35; 112:6; 21:7; 37:24; Mt 6:25-34 Mtwike Bwana fadhaa zako,
naye atakutegemeza,
hatamwacha kamwe mwenye haki wake aanguke.
23 #
Za 5:6; 11:1; 9:15; 73:18; 94:13; 25:2; 30:3; 56:3; Isa 14:15; Eze 28:8; Lk 8:31; Ay 15:32 Lakini wewe, Ee Mungu,
utawashusha waovu katika shimo la uharibifu.
Wenye kiu ya kumwaga damu na wenye hila,
hawataishi nusu ya siku zao.
Lakini mimi ninakutumaini wewe.