Zaburi 99
NEN

Zaburi 99

99
Zaburi 99
Mungu Mfalme Mkuu
1 # 1Nya 16:30, 31; Za 97:1; 2Sam 6:2; Kut 15:14; 25:22 Bwana anatawala,
mataifa na yatetemeke;
anakalia kiti cha enzi katikati ya makerubi,
dunia na itikisike.
2 # Za 48:1; 148:13; 2:6; 46:10; 97:9; 113:4; Kut 15:1 Bwana ni mkuu katika Sayuni;
ametukuzwa juu ya mataifa yote.
3 # Za 103:1; 33:21; 97:12; 76:1; 30:4; 106:47; 111:9; 145:21; 148:5; Kut 15:11 Wanalisifu jina lako ambalo ni kuu na la kuogopwa:
yeye ni mtakatifu!
4 # 1Fal 10:9; Za 98:9; Mwa 18:19, 25; Ufu 15:3; Ay 36:5; Kum 32:3, 4; Isa 11:3-5; Yer 23:5; Za 2:6 Mfalme ni mwenye nguvu na hupenda haki,
wewe umethibitisha adili;
katika Yakobo umefanya
yaliyo haki na sawa.
5 # Isa 66:1; Kut 15:2; 1Nya 28:2; Za 132:7 Mtukuzeni Bwana Mungu wetu,
na mkaabudu katika mahali pa kuwekea miguu yake;
yeye ni mtakatifu.
6 # Kut 24:6; 28:1; 1Sam 7:5; Za 4:3; 91:15 Mose na Aroni walikuwa miongoni mwa makuhani wake,
Samweli alikuwa miongoni mwa walioliitia jina lake;
walimwita Bwana,
naye aliwajibu.
7 # Kut 13:21; 19:9; Hes 11:25; 12:5 Alizungumza nao kutoka nguzo ya wingu;
walizishika sheria zake na amri alizowapa.
8 # Hes 14:20; Sef 3:7; Kum 9:20; Kut 22:27; Law 26:18 Ee Bwana, wetu,
ndiwe uliyewajibu,
kwa Israeli ulikuwa Mungu mwenye kusamehe,
ingawa uliadhibu matendo yao mabaya.
9Mtukuzeni Bwana Mungu wetu,
mwabuduni kwenye mlima wake mtakatifu,
kwa maana Bwana Mungu wetu ni mtakatifu.

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Biblia Takatifu)

Copyright ©1984, 1989, 2009, 2015 by Biblica, Inc.® Used by permission.

All Rights Reserved Worldwide Printed.

Learn More About Neno: Bibilia Takatifu 2014