Zab 12
SUV

Zab 12

12
Ombi la Msaada Wakati wa Dhiki
Kwa mwimbishaji: kwa kufuata Sheminithi. Zaburi ya Daudi.
1 # Isa 57:1 BWANA, uokoe, maana mcha Mungu amekoma,
Maana waaminifu wametoweka katika wanadamu.
2Husemezana yasiyofaa kila mtu na mwenziwe,
Wenye midomo ya kujipendekeza;
Husemezana kwa mioyo ya unafiki;
3BWANA ataikata midomo yote ya kujipendekeza,
Nao ulimi unenao maneno ya kiburi;
4Waliosema, Kwa ndimi zetu tutashinda;
Midomo yetu ni yetu wenyewe,
Ni nani aliye bwana juu yetu?
5 # Kut 3:7,8 Kwa ajili ya kuonewa kwao wanyonge,
Kwa ajili ya kuugua kwao wahitaji,
Sasa nitasimama, asema BWANA,
Nitamweka salama yeye wanayemfyonya.
6 # 2 Sam 22:31; Zab 18:30; Mit 30:5 Maneno ya BWANA ni maneno safi,
Ni fedha iliyojaribiwa kalibuni juu ya nchi;
Iliyosafishwa mara saba.
7Wewe, BWANA, ndiwe utakayetuhifadhi,
Utatulinda na kizazi hiki milele.
8Wasio haki hutembea pande zote,
Ufisadi ukitukuka kati ya wanadamu.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.

Learn More About Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia