Zab 121
SUV

Zab 121

121
Hakikisho la Ulinzi wa Mungu
Wimbo wa Upandaji Mlima.
1Nitayainua macho yangu niitazame milima,
Msaada wangu utatoka wapi?
2Msaada wangu u katika BWANA,
Aliyezifanya mbingu na nchi.
3 # 1 Sam 2:9; Isa 27:3 Asiuache mguu wako usogezwe;
Asisinzie akulindaye;
4Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi,
Yeye aliye mlinzi wa Israeli.
5BWANA ndiye mlinzi wako;
BWANA ni uvuli mkono wako wa kuume.
6 # Isa 49:10 Jua halitakupiga mchana,
Wala mwezi wakati wa usiku.
7 # Ayu 5:19; Zab 91:9,10; Mit 12:21 BWANA atakulinda na mabaya yote,
Atakulinda nafsi yako.
8 # Kum 28:6; Mit 2:8 BWANA atakulinda utokapo na uingiapo,
Tangu sasa na hata milele.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.

Learn More About Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia