Zab 126
SUV

Zab 126

126
Mavuno ya Shangwe
Wimbo wa kupanda mlima.
1 # Mdo 12:9 BWANA alipowarejeza mateka wa Sayuni,
Tulikuwa kama waotao ndoto.
2 # Ayu 8:21 Ndipo kinywa chetu kilipojaa kicheko,
Na ulimi wetu kelele za furaha.
Ndipo waliposema katika mataifa,
BWANA amewatendea mambo makuu.
3BWANA alitutendea mambo makuu,
Tulikuwa tukifurahi.
4Ee BWANA, uwarejeze watu wetu waliofungwa,
Kama vijito vya Kusini.
5 # Isa 12:1-3; Yer 31:9; Yoe 2:17; Mt 5:4; 2 Kor 7:8-11 Wapandao kwa machozi
Watavuna kwa kelele za furaha.
6Ingawa mtu anakwenda zake akilia,
Azichukuapo mbegu za kupanda.
Hakika atarudi kwa kelele za furaha,
Aichukuapo miganda yake.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.

Learn More About Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia