Zab 141
SUV

Zab 141

141
Sala ya Kutaka Kulindwa kutoka kwa Uovu
1Ee BWANA, nimekuita, unijie hima,
Uisikie sauti yangu nikuitapo.
2 # Efe 5:2; 1 Tim 2:8; Ufu 5:8 Sala yangu ipae mbele zako kama uvumba,
Kuinuliwa mikono yangu kama dhabihu ya jioni.
3Ee BWANA, uweke mlinzi kinywani pangu,
Mngojezi mlangoni pa midomo yangu.
4 # Mt 6:14; 20:15; Mit 23:6 Usiuelekeze moyo wangu kunako jambo baya,
Nisiyazoelee matendo yasiyofaa,
Pamoja na watu watendao maovu;
Wala nisile vyakula vyao vya anasa.
5Mwenye haki na anipige, itakuwa fadhili;
Anikemee, itakuwa kama mafuta kichwani;
Kichwa changu kisikatae,
Maana siachi kusali kati ya mabaya yao.
6Makadhi wao wakiangushwa kando ya genge,
Watayasikia maneno yangu, maana ni matamu.
7 # 2 Kor 1:9 Kama kupasua kuni na kuzichanja juu ya nchi,
Ndivyo ilivyo mifupa yetu mdomoni pa kuzimu.
8 # Zab 25:15 Macho yangu yanakuelekea Wewe, MUNGU Bwana,
Nimekukimbilia Wewe, usiniache nafsi yangu.
9Unilinde na mtego walionitegea,
Na matanzi yao watendao maovu.
10 # Est 7:10; Zab 7:15 Wabaya na waanguke katika nyavu zao wenyewe,
Pindi mimi ninapopita salama.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.

Learn More About Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia