Zab 143
SUV

Zab 143

143
Sala ya Ukombozi kutoka kwa Adui
Zaburi ya Daudi.
1Ee BWANA, uisikie sala yangu, uzisikilize dua zangu,
Kwa uaminifu wako unijibu kwa haki yako.
2 # Ayu 14:3; 4:17; Mhu 7:20; Rum 3:20; Gal 2:16 Wala usimhukumu mtumishi wako,
Maana kwako hakuna aliye hai mwenye haki.
3 # Zab 7:1-2 Maana adui ameifuatia nafsi yangu,
Ameutupa chini uzima wangu.
Amenikalisha mahali penye giza,
Kama watu waliokufa zamani.
4 # Zab 61:2 Na roho yangu imezimia ndani yangu,
Moyo wangu ndani yangu umesituka.
5 # Zab 77:5,11 Nimezikumbuka siku za kale,
Nimeyatafakari matendo yako yote,
Naziwaza kazi za mikono yako.
6 # Zab 28:2 Nakunyoshea mikono yangu;
Nafsi yangu inakuonea kiu kama nchi kame.
7Ee BWANA, unijibu hima, roho yangu imelegea;
Usinifiche uso wako,
Nisifanane nao washukao shimoni
8Unifanye kusikia fadhili zako asubuhi,
Kwa maana nimekutumaini Wewe.
Unijulishe njia nitakayoiendea,
Kwa maana nakuinulia nafsi yangu.
9Ee BWANA, uniponye na adui zangu;
Nimekukimbilia Wewe, unifiche.
10 # Zab 25:4; Yn 14:26; Rum 5:5; Efe 4:30; Gal 5:22-23 Unifundishe kuyatenda mapenzi yako,
Kwa maana ndiwe Mungu wangu;
Roho yako mwema aniongoze kwenye nchi sawa,
11Ee BWANA, unihuishe kwa ajili ya jina lako,
Kwa haki yako unitoe roho yangu taabuni;
12Kwa fadhili zako utawakatilia mbali adui zangu;
Na kuwaangamiza wote wanitesao nafsi,
Kwa maana mimi ni mtumishi wako.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.

Learn More About Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia