Zab 150
SUV

Zab 150

150
Sifa kwa Ukuu Mwingi wa Mungu
1Haleluya.
Msifuni Mungu katika patakatifu pake;
Msifuni katika anga la uweza wake.
2Msifuni kwa matendo yake makuu;
Msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.
3Msifuni kwa mvumo wa baragumu;
Msifuni kwa kinanda na kinubi;
4 # Kut 15:20; Isa 38:20 Msifuni kwa matari na kucheza;
Msifuni kwa zeze na filimbi;
5Msifuni kwa matoazi yaliayo;
Msifuni kwa matoazi yavumayo sana.
6 # Ufu 5:13 Kila mwenye pumzi na amsifu BWANA.
Haleluya.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.

Learn More About Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia