Zab 57
SUV

Zab 57

57
Sifa na Hakikisho katika Mateso
Kwa mwimbishaji: kwa mtindo wa Usiharibu. Utenzi wa Daudi alipomponyoka Sauli na kujificha pangoni.
1 # Isa 26:20 Unirehemu, Ee Mungu, unirehemu mimi,
Maana nafsi yangu imekukimbilia Wewe.
Nitaukimbilia uvuli wa mbawa zako,
Hata misiba hii itakapopita.
2 # Zab 138:8 Nitamwita MUNGU Aliye juu,
Mungu anitimiziaye mambo yangu.
3 # Zab 144:5; 40:11 Atapeleka toka mbinguni na kuniokoa,
Atukanapo yule atakaye kunimeza.
Mungu atazipeleka
Fadhili zake na kweli yake
4 # Mit 30:14; Zab 64:3 Nafsi yangu i kati ya simba,
Nitastarehe kati yao waliowaka moto.
Wanadamu meno yao ni mikuki na mishale,
Na ndimi zao ni upanga mkali.
5 # Zab 108:5 Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu,
Na juu ya nchi yote uwe utukufu wako.
6 # Zab 9:15 Wameweka wavu ili kuninasa miguu;
Nafsi yangu imeinama;
Wamechimba shimo mbele yangu;
Wametumbukia ndani yake!
7 # Zab 108:1 Ee Mungu, moyo wangu u thabiti,
Moyo wangu u thabiti.
Nitaimba, nitaimba zaburi,
8 # Amu 5:12 Amka, utukufu wangu.
Amka, kinanda na kinubi,
Nitaamka alfajiri.
9Ee Bwana, nitakushukuru kati ya watu,
Nitakuimbia zaburi kati ya mataifa.
10 # Zab 108:4 Maana fadhili zako ni kubwa hata mbinguni,
Na uaminifu wako hata mawinguni.
11Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu,
Na juu ya nchi yote uwe utukufu wako.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.

Learn More About Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia