Zab 82
SUV

Zab 82

82
Ombi la Kupata Haki
Zaburi ya Asafu.
1 # Mhu 5:8; Kut 21:6 Mungu asimama katika kusanyiko la Mungu;
Katikati ya miungu anahukumu.
2 # Kum 1:17; Zab 58:1,2 Hata lini mtahukumu kwa dhuluma,
Na kuzikubali nyuso za wabaya?
3Mfanyieni hukumu maskini na yatima;
Mtendeeni haki aliyeonewa na fukara;
4Mwokoeni maskini na mhitaji;
Mwopoeni mikononi mwa wadhalimu.
5 # Zab 11:3 Hawajui wala hawafahamu, hutembea gizani;
Misingi yote ya nchi imetikisika.
6 # Ayu 21:32; Eze 31:14; Yn 10:34 Mimi nimesema, Ndinyi miungu,
Na wana wa Aliye juu, nyote pia.
7Lakini mtakufa kama wanadamu,
Mtaanguka kama mmoja wa wakuu.
8 # Zab 2:8; Ufu 11:15 Ee Mungu, usimame, uihukumu nchi,
Maana Wewe utawarithi mataifa yote.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.

Learn More About Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia