Zab 93
SUV

Zab 93

93
Ukuu wa Enzi ya Mungu
1 # Isa 52:7; Ufu 19:6; Ayu 40:10; Zab 104:1; Isa 59:17 BWANA ametamalaki, amejivika adhama,
BWANA amejivika, na kujikaza nguvu.
Naam, ulimwengu umethibitika usitikisike;
2 # Mit 8:22 Kiti chako kimekuwa thabiti tokea zamani;
Wewe ndiwe uliye tangu milele.
3Ee BWANA, mito imepaza,
Mito imepaza sauti zake,
Mito imepaza uvumi wake.
4 # Zab 29:10 Kupita sauti ya maji mengi, maji makuu,
Kupita mawimbi ya bahari yaumkayo,
BWANA Aliye juu ndiye mwenye ukuu.
5Shuhuda zako ni amini sana;
Utakatifu ndio uifaao nyumba yako,
Ee BWANA, milele na milele.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.

Learn More About Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia