Zaburi 131
SRUV

Zaburi 131

131
Kumtumainia Mungu kwa utulivu
Wimbo wa kupanda mlima.
1 # Rum 12:16 BWANA, moyo wangu hauna kiburi,
Wala macho yangu hayainuki.
Wala sijishughulishi na mambo makuu,
Wala mambo yanayozidi nguvu zangu.
2 # Mt 18:3 Hakika nimeituliza nafsi yangu,
Na kuinyamazisha.
Kama mtoto aliyeachishwa kunyonya
Kifuani mwa mama yake;
Roho yangu ni kama mtoto,
Aliyeachishwa kunyonya.
3Ee Israeli, umtarajie BWANA,
Tangu leo na hata milele.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.

Learn More About Swahili Revised Union Version