150
Sifa kwa ukuu Mwingi wa Mungu
1Haleluya.
Msifuni Mungu katika patakatifu pake;
Msifuni katika anga la uweza wake.
2Msifuni kwa matendo yake makuu;
Msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.
3Msifuni kwa mvumo wa baragumu;
Msifuni kwa kinanda na kinubi;
4 #
Kut 15:20; Isa 38:20 Msifuni kwa matari na kucheza;
Msifuni kwa zeze na filimbi;
5Msifuni kwa matoazi yaliayo;
Msifuni kwa matoazi yavumayo sana.
6 #
Ufu 5:13
Kila mwenye pumzi na amsifu BWANA.
Haleluya.