Zaburi 126
BHNTLK

Zaburi 126

126
Kuomba nguvu mpya#126 Mazingira ya Zaburi hii ni yale ya wakati mara baada ya kurudi kutoka uhamishoni Babuloni. Zaburi yenyewe ina sehemu mbili: Ya kwanza (126:1-3) watu wanakumbuka Mungu alivyowaokoa wakati mmoja; na ya pili (126:4-6) wanamwomba afanye vivyo hivyo hata wakati huo.
(Wimbo wa Kwenda Juu)
1Mwenyezi-Mungu alipoturekebisha na kuturudisha Siyoni,#126:1 Alipoturekebisha na kuturudisha Siyoni: Maneno haya aghalabu yahusu Waisraeli waliporudi kutoka uhamishoni kule Babuloni.
tulikuwa kama watu wanaoota ndoto!
2Hapo tuliangua kicheko;
tulishangilia kwa furaha.
Nao watu wa mataifa mengine walisema:
“Mwenyezi-Mungu amewatendea mambo makubwa!”
3Kweli Mwenyezi-Mungu alitutendea mambo makubwa,
tulifurahi kwelikweli!
4Ee Mwenyezi-Mungu, urekebishe tena hali yetu,
kama mvua inavyotiririsha maji katika mabonde makavu.
5Wanaopanda kwa machozi,
watavuna kwa shangwe.
6Wanaokwenda kupanda mbegu wakilia,
watarudi kwa furaha wakichukua mavuno.#126:6 Maneno mwafaka kabisa ambayo kwa picha kamili yanaonesha jinsi watu wa Mungu walivyo na matumaini hata wakati wa magumu ya maisha.

Copyright The Bible Society of Tanzania, 1993

The Bible Society of Kenya 1993

Learn More About Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza