Zaburi 134
BHNTLK

Zaburi 134

134
Msifuni Mungu#134 Zaburi hii ni ya mwisho ya fungu la zaburi zenye anwani “Wimbo wa Kwenda Juu” (taz Zab 120).
(Wimbo wa Kwenda Juu)
1Njoni kumsifu Mwenyezi-Mungu enyi watumishi wake wote,
enyi nyote mnaotumikia usiku nyumbani mwake.
2Inueni mikono kuelekea mahali patakatifu,
na kumtukuza Mwenyezi-Mungu!
3Mwenyezi-Mungu awabariki kutoka Siyoni;#134:3 Mwenyezi-Mungu awabariki kutoka Siyoni: Maneno haya huenda yalitamkwa na kuhani kuwatakia baraka mahujaji waliofika Yerusalemu kwa sikukuu fulani. Taz pia 104.
yeye aliyeumba mbingu na dunia.

Copyright The Bible Society of Tanzania, 1993

The Bible Society of Kenya 1993

Learn More About Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza