Mithali 29
NMM

Mithali 29

29
1 # 2Nya 36:16; Mit 6:15 Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi,
ataangamia ghafula, wala hapati dawa.
2 # 2Fal 11:20; Es 8:15; Mit 28:12 Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi;
waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.
3 # 1Fal 1:48; Mit 10:1; 23:15-16; 5:8-10; Lk 15:11-32 Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake,
bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.
4 # Mit 8:15-16 Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti,
bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.
5 # Ay 32:21; Mit 26:28 Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili,
anautandaza wavu kuitega miguu yake.
6 # Ay 5:13; Mhu 9:12 Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe
bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.
7 # Ay 29:16; Za 41:1; Isa 35:3-4 Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini,
bali mwovu hajishughulishi na hilo.
8 # Mit 11:11; 16:14 Wenye mzaha huuchochea mji,
bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.
9 # Mt 11:17 Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu,
mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.
10 # Mwa 4:5-8; 1Yn 3:12 Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu
na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
11 # Ay 15:13; Mit 12:16 Mpumbavu huonyesha hasira yake yote,
bali mwenye hekima hujizuia.
12 # 2Fal 21:9; Ay 34:30 Kama mtawala akisikiliza uongo,
maafisa wake wote huwa waovu.
13 # Mit 22:2; Mt 5:45 Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili:
Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
14 # Mit 29:4; Za 72:1-5; Mit 16:12 Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki,
kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
15 # Mit 29:17; 13:24 Fimbo ya maonyo hutia hekima,
bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo
humwaibisha mama yake.
16 # Za 37:36; 58:10; 91:8 Wakati waovu wanapostawi,
pia dhambi vivyo hivyo,
lakini wenye haki wataliona anguko lao.
17 # Mit 13:24; 29:15 Mrudi mwanao, naye atakupa amani,
atakufurahisha nafsi yako.
18 # Za 19:11; Yn 13:17; Amo 8:11-12; 1Sam 3:1 Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia,
bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
19Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu,
ajapoelewa, hataitikia.
20 # Mit 14:17 Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka?
Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
21Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani,
atamletea sikitiko mwishoni.
22 # Mit 14:17 Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi,
naye mtu mwenye hasira ya haraka
hutenda dhambi nyingi.
23 # Isa 66:2; Mt 23:12; Yak 4:6 Kiburi cha mtu humshusha,
bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu
hupata heshima.
24 # Law 5:1 Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe;
huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
25 # 1Sam 15:24; Mit 28:25; 16:20 Kuwaogopa watu huwa ni mtego,
bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
26 # Mit 19:6; 16:33 Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala,
bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
27 # Mit 29:10 Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu;
waovu huwachukia sana wenye haki.

Kiswahili Contemporary Scriptures (Neno: Maandiko Matakatifu)

Copyright © 2018 by Biblica, Inc.®

All Rights Reserved Worldwide.

Learn More About Neno: Maandiko Matakatifu