Nahumu UTANGULIZI
SCLDC10

Nahumu UTANGULIZI

UTANGULIZI
Kijitabu hiki cha Nahumu kinatangaza kuteketezwa kwa Ninewi, mji mkuu wa utawala wa Ashuru. Nahumu anatabiri na kueleza kwa ufasaha sana maangamizi hayo hata anajulikana kama mmoja wa washairi maarufu wa Israeli. Kuanguka kwa Ninewi ni adhabu kutoka kwa Mungu ambaye huwaadhibu wote wanaopinga matakwa yake: 1:11; 2:1. Kitabu kinasisitiza na kutilia mkazo kwamba Mwenyezi-Mungu hauadhibu udhalimu, ukatili na maisha ovyo ya watu.

Swahili Common Language DC Bible: Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki © Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya, 1995, 2001. Haki zote zimehifadhiwa.  

Learn More About BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA