Zaburi 12
SCLDC10

Zaburi 12

12
Kuomba msaada
(Kwa Mwimbishaji: Mtindo wa Sheminithi. Zaburi ya Daudi)
1Fanya haraka, ee Mwenyezi-Mungu!
Watu wema wamekwisha;
waaminifu wametoweka miongoni mwa watu.
2Kila mmoja humdanganya mwenzake,
husema kwa kudanganya na kwa moyo wa unafiki.
3Ee Mwenyezi-Mungu
uikomeshe hiyo midomo ya udanganyifu,
na ndimi hizo zinazojigamba kupindukia.
4Wao husema: “Kwa ndimi zetu tutashinda;
midomo tunayo, nani awezaye kututawala?”
5Lakini Mwenyezi-Mungu asema:
“Kwa sababu maskini wanadhulumiwa,
na wahitaji wanapiga kite, sasa naja,
nami nitawapa usalama wanaoutazamia.”
6Neno la Mwenyezi-Mungu ni safi,
safi kama fedha iliyosafishwa katika tanuri,
naam, kama fedha iliyosafishwa mara saba.
7Utulinde, ee Mwenyezi-Mungu,
utukinge daima na kizazi hiki kiovu.
8Waovu wanazunguka kila mahali;
upotovu unatukuzwa kati ya watu.

Swahili Common Language DC Bible: Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki © Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya, 1995, 2001. Haki zote zimehifadhiwa.  

Learn More About BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA