Zaburi 123
SCLDC10

Zaburi 123

123
Kuomba huruma
(Wimbo wa Kwenda Juu)
1Nakutazamia kwa hamu, ee Mwenyezi-Mungu,
nakuangalia wewe utawalaye huko juu mbinguni!
2Kama watumishi wamtegemeavyo bwana wao,
kama mjakazi amtegemeavyo bibi yake,
ndivyo nasi tunavyokutegemea wewe,
ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu,
mpaka hapo utakapotuonea huruma.
3Utuhurumie, ee Mwenyezi-Mungu, utuhurumie,
maana tumedharauliwa kupita kiasi.
4Tumeshiba muda mrefu dharau za matajiri,
tumepuuzwa mno na wenye kiburi.

Swahili Common Language DC Bible: Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki © Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya, 1995, 2001. Haki zote zimehifadhiwa.  

Learn More About BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA