Zaburi 128
SCLDC10

Zaburi 128

128
Tuzo kwa jamaa imchayo Mungu
(Wimbo wa Kwenda Juu)
1Heri wote wamchao Mwenyezi-Mungu,
wanaoishi kufuatana na amri zake.
2Utapata matunda ya jasho lako,
utafurahi na kupata fanaka.
3Mkeo atakuwa kama mzabibu wa matunda mengi nyumbani mwako;
watoto wako kama chipukizi za mzeituni kuzunguka meza yako.
4Naam, ndivyo atakavyobarikiwa
mtu amchaye Mwenyezi-Mungu.
5Mwenyezi-Mungu akubariki kutoka Siyoni!
Uione fanaka ya Yerusalemu, siku zote za maisha yako.
6Uishi na hata uwaone wajukuu zako!
Amani iwe na Israeli!

Swahili Common Language DC Bible: Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki © Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya, 1995, 2001. Haki zote zimehifadhiwa.  

Learn More About BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA