Zaburi 131
SCLDC10

Zaburi 131

131
Kumtumainia Mungu kwa utulivu
(Wimbo wa Kwenda Juu, wa Daudi)
1Ee Mwenyezi-Mungu, sina moyo wa kiburi;
mimi si mtu wa majivuno.
Sijishughulishi na mambo makuu,
au yaliyo ya ajabu mno kwangu.
2Ila nafsi yangu imetulia na kuwa na amani,
kama mtoto mchanga alivyotulia na mama yake;
ndivyo nafsi yangu ilivyo tulivu.
3Ee Israeli, umtumainie Mwenyezi-Mungu,
tangu sasa na hata milele.

Swahili Common Language DC Bible: Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki © Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya, 1995, 2001. Haki zote zimehifadhiwa.  

Learn More About BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA