Zaburi 150
SCLDC10

Zaburi 150

150
Zaburi ya kumsifu Mungu
1Msifuni Mwenyezi-Mungu!
Msifuni Mungu katika patakatifu pake;
msifuni katika mbingu zake kuu.
2Msifuni kwa sababu ya matendo yake makuu;
msifuni kwa ajili ya utukufu wake mkuu.
3Msifuni kwa mlio wa tarumbeta;
msifuni kwa zeze na kinubi!
4Msifuni kwa ngoma na kucheza;
msifuni kwa filimbi na banjo!
5Msifuni kwa kupiga matoazi.
Msifuni kwa matoazi ya sauti kubwa.
6Kila kiumbe hai kimsifu Mwenyezi-Mungu!
Msifuni Mwenyezi-Mungu!

Swahili Common Language DC Bible: Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki © Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya, 1995, 2001. Haki zote zimehifadhiwa.  

Learn More About BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA